Forum Navigation
You need to log in to create posts and topics.

Ifahamu sumu inayopatikana kwenye mihogo

Sumu ya cyanide ni tatizo linaloweza kutokea kutokana na ulaji wa mihogo, hasa aina ya mihogo michungu. Sumu hii inatokana na kemikali iitwayo cyanogenic glycosides, ambayo inapokuwa mwilini hugeuka kuwa cyanide , kemikali hatari kwa afya ya binadamu.

Wakati ambao Sumu Huzidi

Mihogo michungu: Ina kiwango kikubwa cha cyanogenic glycosides ikilinganishwa na mihogo tamu.

Ukame: Hali ya hewa ya ukame huongeza kiwango cha sumu kwenye mihogo.

Maandalizi duni: Mihogo isiyopikwa vizuri au kutayarishwa kwa usahihi inaweza kuwa hatari.

Tahadhari ni muhimu ili kuhakikisha mihogo ni salama kwa ulaji!

error: Content is protected !!